you are a man, you have the ability to pursue your dreams, and you are so powerful

Monday, April 21, 2014

Tagged Under:

MWANAUME,TOKA GEREZA LA FIKRA.

Share

Hakuna mtu aliyeumbwa ili afanye makosa,kila mtu ameumbwa ili aishi katika viwango vya juu vya maisha na kutimiza kusudi la maisha,mtu anapoishi katika viwango vya juu na kutimiza kusudi la maisha,huyafurahia maisha na kuona maisha ni ya thamani.
Ni hulka ya mwanadamu kujaribu vitu vingi katika maisha yake, haswa vijana hupenda kudadisi na kujaribu mambo mengi katika maisha, Albert Einstein alipata kusema “Kama haujawai kufanya kosa lolote,basi haujawai kujaribu kitu chochote”,kwa mantiki hiyo mtu anayejaribu vitu vingi,hufanya makosa mengi.
 Katika kutimiza ndoto ya maisha yako,utajaribu vitu vingi,na katika majaribio hayo kuna makosa utakayo yafanya,na haina maana kwamba uishie hapo hapo pindi unapofanya makosa ,bali unapaswa kujifunza kutoka katika makosa hayo,unapojifunza kutoka katika makosa,una jenga hali na ufahamu wa kutokurudia makosa yale yale,watu wengi wanarudia makosa mara nyingi,kwasababu tu hawana utaratibu wa kujifunza katika makosa yao,leo hii thubutu kujifunza katika makosa yako,na si kujiona mtu usiyefaa.
Achilia mbali makosa yanayofanywa na mtu anapotaka kutimiza ndoto zake,kuna makosa ambayo mtu hufanya katika maisha yake ya kila siku,aidha kwa kukusudia au kwa kutokusudia,baada ya mtu kufanya makosa mara nyingi mtu hujisikia ana hatia(guilty),wapo watu wanaotubu na wengine wala hata hawatubu,wapo naojisamehe nafsi zao na wapo ambao hawajisamehi nafsi zao.
 Mtu anapokuwa na hatia hupoteza hamu ya kufanya mambo makubwa (Extra ordinary things), leo hii tuna watu wengi sana wanaoteswa na hisia za mambo waliyofanya katika maisha yao,hawawezi kuelezea na wala hawajui wa anzaje kueleza,wana ndoto,lakini kuta za gereza la fikra zimewazui wasitimize ndoto zao,tuna waona wanafuraha na Amani lakini kiukweli hawana,wamefungwa kisawa sawa.
Mimi sijui upo gereza gani, ni wewe tu ndiye unayejua, na tena unajua umekaa gerezani kwa siku ngapi, wiki nagapi, miezi mingapi, miaka mingapi? Hauwezi ukawa huru kama hisia za makosa zimekufunguka, ni lazima utoke huko, kwani tangu umekuwa kwenye hilo gereza umefaidika na nini? hakuna ulichopata Zaidi ya hisia za maumivu.
Ndoto uliyo nayo ni kubwa sana,muda wakuanza kuitekeleza ni sasa,ili uweze kuitekeleza ni lazima utoke gerezani,utakapotimiza ndoto yako utayabadilisha maisha yako na maisha ya watu wengine. Wakati wako ni sasa, toka huko kwenye maumivu ya hisia za makosa,na uishi maisha  yenye furaha siku zote.
Kwa msaada na ushauri
Na Baraka Daniel
+255762362413


0 comments:

Post a Comment

Need an Inspiration?

We have competant speakers on men issues,please contact with us

Name Email * Message *

Our Location